Pages

Sunday, May 5, 2013

MOUNTAIN DEW Yakatisha DEAL Yake Na LIL WAYNE ...


Rick Ross amekuwa sio wa kwanza baada ya deal yake na REEBOK kukatishwa baada ya kuandika mashairi yake yanayochochea vitendo vya ubakaji ... LIL WAYNE amefuatia ... hii ni baada ya MOUNTAIN DEW kumuadhibu kwa kukatisha deal yao baada ya mistari yake iliyomgusa mwanaharakati wa haki za kiraia Emmett Till.
“Beat that pu**y up like Emmitt Till,” ame-rap LIL WAYNE, rapper kutoka New Orleans katika original remix ya ngoma ya Future inayojulikana kama “Karate Chop.”
According to LIL WAYNE, mistari hiyo ilifutwa baadae na yeye kutuma barua kwa familia ya mwanaharakati huyo na kuomba msamaha lakini hii haikutosha ...
Emmitt Louis Till alikuwa ni mvulana mwenye asili ya kaifrika nchini Marekani ambaye aliuawa huko Mississippi akiwa na umri wa miaka 14 baada ya kubainika kuwa na mwanamke mweupe ...
Pamoja na kuyatoa, familia ya TILL imekuja juu na kumshutumu LIL WAYNE kwa matumizi ya jina hilo la ndugu yao ...
Viongozi wa Mountain Dew walichukua maamuzi siku ya Ijumaa na kutangaza kukatisha mkataba huo na LIL WAYNEmwenye miaka 30 sasa ...
Ndugu wa Emmitt Louis Till wameomba mkutano na rapper huyo baada ya barua iliyotumwa na Lil Wayne ili kuweza ku-discuss makubaliano kati ya rapper huyo na uongozi wa PepsiCo ...