Pages

Monday, July 15, 2013

Huyu ndiye model wa Tanzania aliyepata dili ya kutangaza nguo na viatu vya kampuni ya Adidas.



Jina lake anaitwa Danny David ni Mwanamitindo wa kume toka Tanzania na mwanamitindo pekee toka Tanzania alipata nafasi ya kufanya kazi ya kutangaza nguo na viatu vya kampuni kubwa ya Adidas tawi la Afrika ya kusini. 

Alianza kuonekana kwenye fashion mwaka 2012 kwenye maonesho ya Swahili Fashion Week chini ya mwanamitindo maarufu nchini Mustapha Hasanali, ameshiriki kuonesha mavazi kwenye Harusi fashion week iliyofanyika chini ya mbunifu wa mavazi Ally Rehmutula na pia alishawahi kushiriki na kushinda kwenye mashindano ya wanamitindo ya Maridadi model search yaliyofanyika hapa Tanzania.

Danny ni mwanasheria kitaaluma na ana degree ya sharia toka chuo cha Tumaini Iringa


Katika interview tuliyofanya naye hivi karibuni Danny amesema pamoja na kuwa mwanamitindo anamipango ya kuwa muigizaji kwani ni kitu alichokuwa anapenda kukifanya tangu utotoni.