Pages

Friday, April 12, 2013

LUCY KOMBA NDANI YA "FROM TANZANIA TO DENMARK" NI BALAA.....KARIBU NIKUPEKULIE




Lucy Komba actress mwenye jina kubwa Swahiliwood anakuja kivingine katika filamu mpya inayoitwa "From Tanzania To Denmark" ambayo  imetengenezwa katika nchi hizi mbili huku ikishirikisha waigizaji wa Tanzania na wengine kutoka Denmark ambao wengine wana asili ya kiafrika na wengine asili ya Denmark. Waigizaji hao ni kama Selembe Toko na Maggie Moreno.

 Filamu inahusu binti mmoja(Lucy Komba) kutoka kijijini anakuja Dar es salaam ili aende Denmark lakini kutokana na vituko vyake akiwa mshamba wa kupitiliza ndiyo itakufanya uwe na hamu ya kuitizama filamu hii ili  umuone binti huyo atakuwaje na ushamba wake huko Debnmark kama akiwa Dar-es salaam tu anafanya drama za kufa mtu. 

 Lucy now yupo katika maandalizi ya kwenda Denmark ambapo filamu hii itazinduliwa huko ambapo ameshirikiana na kampuni yaVad Production katika kuiandaa na tayari imeshakamilika. Kaa mkao wa kula usikose filamu hii

Mbali  na  balaa  hilo, Vad Production  imekwisha  kamilisha filamu  yake  mpyaaaa  iitwayo  "IF I KNEW" ambayo  itaingia sokoni  siku  ya  jumatatu....

Filamu  hiyo  ya  kimataifa  imewashirikisha  wakali  wa  filamu  duniani  kama  SAFARI LUKEKA ,TANTINE DANIEL MUSA, FRANK SALUMU  na ELIANE KISONGA

Kazi  kwao  mdau  wa  filamu.

HII  NI  TRAILER  YA  FILAMU  HIYO