
kutoka
Nigeria,
Goldie Harvey famously known as
"Goldie" anataraji kutengeneza album ambayo itagusa kila kona ya
Africa.
Goldie ambae pia alikuwa mshiriki wa shindano la
Big Brother Africa la mwaka jana ameyasema hayo katika interview aliyofanya na
MTVBase Africa hivi karibuni.

Katika kufanikisha hilo,
Goldie anataraji kufanya album hiyo ambayo bado hajaipatia jina na atleast wasanii 10 bora kutoka
Africa ambapo mpaka sasa ameshafanya singles tatu ambazo zitatangulia, ikiwemo
SKIBOBO featuring
AY (@AyTanzania) kutoka
Tanzania, MILIKI feat.
Navio kutoka
Uganda na
GIVE IT TO ME akimshirikisha
J.Martinskutoka
Nigeria.
Goldie amekuwa akifanya vizuri sana kwenye muziki hasa baada ya kutoka kwenye Jumba la
BBA-StarGame mwaka jana, ngoma zake zikisikilizwa sana
Africa na duniani pia.