Pages

Wednesday, February 27, 2013

Chris Brown Na Rihanna Kufunga Ndoa Ifikapo July Mwaka Huu...???


Mastar wawili kutoka nchini Marekani, Chris Brown na mpenzi wake Rihanna wameripotiwa kupanga kufunga ndo ifikapo July mwaka huu.
Jarida moja maarufu sana la nchini Marekani liitwalo ''Star Magazine'' limeripoti kuwa mastaa hao wana tarajia kufunga ndoa ifikapo July mwaka huu katika visiwa vya Barbados.
Kwa mara ya kwanza wawili hao wamepanga kufunga ndoa hiyo ambayo itakuwa ya kitofauti ikiwa na watu wa karibu ambao wanaamini Chris Breezy amebadilika kweli na upendo wa dhati kwa Rihanna hasa baada ya tukio alilolifanya mwaka 2009.
Mwaka 2009, Chris Brown alimpiga mwanadada Rihanna na ku-make headlines kubwa sana iliyopelekea watu wengi kumchukia ikiwemo kushtakiwa kutokana na kitendo hicho.