Pages

Tuesday, February 26, 2013

HILI NDIO GARI LILILONUNULIWA NA MCHEKESHAJI STAA WA NIGERIA, ALITOA ODA KIWANDANI.


.Huu ndio mkoko mpya ambao model yake ni ya 2013, ni Opel Insignia na bei yake ni pound elfu 42.
2013 unazidi kuwa mwaka wa mastaa wa Nigeria kununua magari ya kifahari na yaliyotengenezwa hivi karibuni ambapo leo kwenye headlines muhusika mkuu ni mchekeshaji aitwae Basket Mouth akiwa ni staa ambae Nigeria imemfahamu kutokana na uchekeshaji wake.
Imeripotiwa na Linda kwamba hili gari Basket alitoa oda kiwandani na hakuna gari kama hili Africa ikiwa ni siku chache tu amelinunua baada ya kukamilisha ujenzi wa hii nyumba hapa chini ya mamilioni ya Naira zawadi kwa mama yake mzazi maarufu kama Madam Okpocha.