Pages

Tuesday, February 19, 2013

FIFA YATHIBITISHA MATUMIZI YA GOAL-LINE TECHNOLOGY KOMBE LA DUNIA BRAZIL.



Shrikisho la soka duniani FIFA limepitisha matumizi ya kutumia teknolojia ya kuthibitisha mpira kuvuka mstari na kuingia golini ( Goal-line Teknoloji 'GTL') katika fainali ya kombe la dunia nchini Brazil 2014.
Teknoloji hiyo pia imethibitishwa kuwa itatumika katika michuano ya kombe la shirikisho ambayo itaanza kutimua vumbi June 15 mwaka huu.
Taarifa iliyochapishwa katika mtandao wa shirikisho hilo imesema
"Baada ya jitihada za kuhakikisha teknolojia hiyo inajaribiwa na kuona kama inafaa kupitia michuano ya kombe la dunia la vilabu nchini Japan Desemba mwaka jana 2012, FIFA imeamua kuanza kutumia GTL katika michuano ya kombe la shirikisho nchini Brazil june 2013 and baadaye fainali ya FIFA ya kombe la dunia 2014 nchini Brazil.
Imekaririwa taarifa hiyo ikisema
"Lengo ni kutumia GLT ili kusaidia waamuzi na kupanda mfumo katika viwanja vyote”
FIFA pia imezindua zabuni ya imealika watu wote wenye kutengeneza na kutoa huduma ya mfumo huo wa goal-line technology kuomba kupewa kandarasi hizo huku maamuzi ya aliyeshinda yakitarajiwa kutolewa mwezi April.
Mifumo ya Hawk-Eye na GoalRef yote tayari imepitishwa na  FIFA, ambayo inatumia kamera ikihusisha nguvu ndogo za mafasa ya kunasa nguvu za sumaku kuzunguka goli ambapo ndani ya mipira kutakuwa na saketi inayowashwa kwa lengo la kunasa mawasiliano(siyo tafsiri rasmi).

Alves anamtaka Neymar ajiunge na Barcelona.
 Mlinzi wa kimataifa wa Brazil na Barcelona Dani Alves amemtaka mshambuliaji wa Santos na timu ya taifa ya Brazil kujiunga naye katika timu yake ya Barcelona wakati huu ambapo kuna tetesi kuwa kigogo hicho cha Hispania kinatengeneza mazingira mazuri ya kujenga hatma njema ya baadaye ya kinda huyo.
Neymar amekuwa mchezaji bora kwa miaka miwili mfululizo wa bara la Amerika Kusini.
Alves alishindwa kuficha juu ya hisia zake katika jaribio lake la kuendelea kumshawishi Neymar mwenye umri wa miaka 20 kujiunga Nou Camp.
Lakini wakati tetesi nyingine juu ya mshambuliaji huyo kutaka kuelekea Ulaya baada ya michuano ya kombe la dunia mwakani na kujiunga na Manchester City au Bayern Munich kama ilivyokuwa inaarifiwa , Alves anasema atahakikisha mipango hiyo inashindwa