Pages

Tuesday, February 5, 2013

Prezzo Kufunga Ndoa Na Goldie Mwezi Huu...


Rapper maarufu kutoka nchini KenyaCMB Prezzo ambae pia alikuwa ni mmoja wa washiriki wa Big Brother Africa 2012 [StarGame] sasa anatarajia kufunga pingu za maisha na mwanadada ambae pia alishiriki shindano hilo mwaka huo huo, Goldie Harvey ambae alikuwa ni mshiriki kutoka Nigeria.
Prezzo alianza kujihusisha kimapenzi na Goldie wakiwa katika jumba hilo ingawa hawakuonekana serious sana. Mara kadhaa Goldie amekuwa akiulizwa na kukana mahusiano hayo hadi hivi karibuni iliporipotiwa kuwa Prezzo alienda mjiniLagos, Nigeria ambako inapoishi familia ya Goldie na kwenda kutoa barua ya kutaka kumuoa.
Taarifa hizo zimetolewa na mtandao wa Big Brother na kusema kuwa wawili hao wamemua kufunga ndoa yao hiyo siku ya Jumapili ya tarehe 9 February mwaka huu mjini Lagos, Nigeria.