Pages

Friday, March 8, 2013

AIBU: PICHA ZA UCHI ZA MISS KINONDONI NAMBA2 ZANASWA



Miss Dar Indian Ocean ambaye ni Miss Kinondoni namba 2 mwaka jana, Diana Hussein  hivi karibuni amejikuta akipata aibu baada ya picha yake ya utupu kuvuja...
  
Picha hiyo inayomuonesha Diana akiwa matiti nje, imesambaa kwenye mtandao wa simu wa BBM huku baadhi ya watu ‘wakifoadiana’. 

Baadhi ya marafiki wa mrembo huyo walisema kuwa wameshangaa kuiona picha hiyo kwani kwa wanavyomjua hawakutarajia.

Akiizungumzia picha hiyo, Diana alisema aliipiga kwa matumizi yake binafsi ila akashangaa kuona imesambaa mtandaoni.

Wakati Diana akiteswa na skendo hiyo, Miss Rukwa namba 3 mwaka jana, Vency Edward naye amefuata mkumbo baada ya picha zake za utupu kunaswa.

Picha hizo kama ilivyo kwa Diana, zimezagaa kwenye mtandao wa BBM na zinamuonesha ameshusha gauni lake hadi kiunoni na kuliacha eneo la juu wazi.

Haikuweza kufahamika mara moja za sababu za yeye kupiga picha hizo na jitihada za kumtafuta zinaendelea ili aweze kuzifungukia.